< Zaburi 57 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
For the leader. Al tashheth. A michtam of David, when he fled from Saul into a cave. Be gracious, O God, be gracious to me, for in you I take shelter. In your sheltering wings I take refuge, till ruin be over past.
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
I cry to the Most High God, to the God who accomplishes for me.
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
He will send me his succour from heaven, he will thrust away those who would trample me. (Selah)
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
In the midst of lions I lie, who devour human prey. Their teeth are spears and arrows, and their tongue is a sharpened sword.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Be exalted, God, o’er the heavens, and your glory o’er all the earth.
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
They set a net for my feet, but in it was their own foot caught. Before me they dug a pit, but they fell into it themselves. (Selah)
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
My heart is steadfast, O God, my heart is steadfast. I would sing, I would make music;
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
awake, my soul. Awake, harp and lyre; I would wake the dawn.
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I would praise you among the peoples, O Lord, and make music among the nations to you;
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
for great to heaven is your love, and your faithfulness to the clouds.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Be exalted, God, o’er the heavens, and your glory o’er all the earth.

< Zaburi 57 >