< Zaburi 57 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
Be merciful unto me, O God, be merciful unto me: for my soul trusts in you: yea, in the shadow of your wings will I make my refuge, until these calamities pass over.
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
I will cry unto God most high; unto God that performs all things for me.
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
He shall send from heaven, and save me from the reproach of him that would swallow me up. (Selah) God shall send forth his mercy and his truth.
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
My soul is among lions: and I lie even among them that are set on fire, even the sons of men, whose teeth are spears and arrows, and their tongue a sharp sword.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Be you exalted, O God, above the heavens; let your glory be above all the earth.
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
They have prepared a net for my steps; my soul is bowed down: they have dug a pit before me, into the midst whereof they are fallen themselves. (Selah)
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
My heart is fixed, O God, my heart is fixed: I will sing and give praise.
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Awake up, my glory; awake, psaltery and harp: I myself will awake early.
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I will praise you, O Lord, among the people: I will sing unto you among the nations.
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
For your mercy is great unto the heavens, and your truth unto the clouds.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Be you exalted, O God, above the heavens: let your glory be above all the earth.

< Zaburi 57 >