< Zaburi 57 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
Unto the end. May you not destroy. Of David, with the inscription of a title, when he fled from Saul into a cave. Be merciful to me, O God, be merciful to me. For my soul trusts in you. And I will hope in the shadow of your wings, until iniquity passes away.
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
I will cry out to God Most High, to God who has been kind to me.
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
He sent from heaven and freed me. He has surrendered into disgrace those who trampled me. God has sent his mercy and his truth.
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
And he has rescued my soul from the midst of the young lions. I slept troubled. The sons of men: their teeth are weapons and arrows, and their tongue is a sharp sword.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Be exalted above the heavens, O God, and your glory above all the earth.
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
They prepared a snare for my feet, and they bowed down my soul. They dug a pit before my face, yet they have fallen into it.
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
My heart is prepared, O God, my heart is prepared. I will sing, and I will compose a psalm.
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Rise up, my glory. Rise up, psaltery and harp. I will arise in early morning.
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I will confess to you, O Lord, among the peoples. I will compose a psalm to you among the nations.
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
For your mercy has been magnified, even to the heavens, and your truth, even to the clouds.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Be exalted above the heavens, O God, and your glory above all the earth.