< Zaburi 57 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
To the chief music-maker; put to Al-tashheth. Michtam. Of David. When he went in flight from Saul, in the hole of the rock. Have mercy on me, O God, have mercy on me; for the hope of my soul is in you: I will keep myself safely under the shade of your wings, till these troubles are past.
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
I will send up my cry to the Most High God; to God who does all things for me.
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
He will send from heaven, and take me from the power of him whose desire is for my destruction. God will send out his mercy and his good faith.
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
My soul is among lions; I am stretched out among those who are on fire, even the sons of men, whose teeth are spears and arrows, and whose tongue is a sharp sword.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
O God, be lifted up higher than the heavens; let your glory be over all the earth.
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
They have made ready a net for my steps; my soul is bent down; they have made a great hole before me, and have gone down into it themselves. (Selah)
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
My heart is fixed, O God, my heart is fixed; I will make songs, and give praise.
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
You are my glory; let the instruments of music be awake; I myself will be awake with the dawn.
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I will give you praise, O Lord, among the peoples; I will make songs to you among the nations.
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
For your mercy is great, stretching up to the heavens, and your righteousness goes up to the clouds.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Be lifted up, O God, higher than the heavens, let your glory be over all the earth.

< Zaburi 57 >