< Zaburi 57 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
(Til sangmesteren. Al-tasjhet. Af David. En miktam, da han flygtede ind i hulen for Saul.) Vær mig nådig, Gud, vær mig nådig, thi hos dig har min Sjæl søgt Ly; i dine Vingers Skygge søger jeg Ly, til Ulykken er drevet over.
2 Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
Gud, den Højeste, påkalder jeg, den Gud, der gør vel imod mig;
3 Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
han sender mig Hjælp fra Himlen og frelser min Sjæl fra dem, som vil mig til Livs. Gud sender sin Nåde og Trofasthed.
4 Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
Jeg må ligge midt iblandt Løver, bo mellem Folk, der spyr Ild, hvis Tænder er Spyd og Pile, hvis Tunge er hvas som et Sværd.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Løft dig, o Gud, over Himlen, din Herlighed være over al Jorden!
6 Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
Et Net har de udspændt for mine Skridt, deres egen Fod skal hildes deri; en Grav har de gravet foran mig, selv skal de falde deri. (Sela)
7 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
Mit Hjerte er trøstigt, Gud, mit Hjerte er trøstigt; jeg vil synge og lovprise dig,
8 Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
vågn op, min Ære! Harpe og Citer vågn op, jeg vil vække Morgenrøden.
9 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
Jeg vil takke dig, Herre, blandt Folkeslag, prise dig blandt Folkefærd;
10 Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
thi din Miskundhed når til Himlen, din Sandhed til Skyerne.
11 Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.
Løft dig, o Gud, over Himlen, din Herlighed være over al Jorden!