< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
Al Vencedor: sobre la paloma silenciosa en paraje muy distante. Mictam de David, cuando los filisteos le prendieron en Gat. Ten misericordia de mí, oh Dios, porque me devoraría el hombre; me oprime combatiéndome cada día.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Me devoran mis enemigos cada día; porque muchos son los que pelean contra mí, oh Altísimo.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
El día temo, mas yo en ti confío.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
En Dios alabaré su palabra; en Dios he confiado, no temeré lo que la carne me hiciere.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
Todos los días me contristan mis negocios; contra mí son todos sus pensamientos para mal.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
Se reúnen, se esconden, miran ellos atentamente mis pisadas, esperando mi alma.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
¿Escaparán ellos por la iniquidad? Oh Dios, derriba los pueblos con tu furor.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
Mis huidas has contado tú; pon mis lágrimas en tu odre, ciertamente en tu libro.
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Entonces serán vueltos atrás mis enemigos el día que yo clamare a ti; en esto conozco que Dios es por mí.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
En Dios alabaré su palabra; en el SEÑOR alabaré su palabra.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
En Dios he confiado; no temeré lo que el hombre me pueda hacer.
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
Sobre mí, oh Dios, están tus promesas; te tributaré alabanzas.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Porque has librado mi vida de la muerte, ciertamente mis pies de caída, para que ande delante de Dios en la luz de los que viven.

< Zaburi 56 >