< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
Jusqu'à la Fin, pour le peuple, quand il fut éloigné des saints lieux, inscription de David, lorsque les Philistins l'eurent maîtrisé dans Geth. Aie pitié de moi, ô Dieu, car l'homme m'a foulé aux pieds; tout le jour, il a bataillé contre moi, et il m'a accablé.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Mes ennemis m'ont foulé aux pieds tout le jour, à partir de l'aurore; ils étaient nombreux à me combattre.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
Mais ils sentiront la crainte, et moi j'espérerai en toi.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
En Dieu je louerai mes paroles; tout le jour j'ai espéré en Dieu; je ne craindrai rien de ce que la chair fera contre moi.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
Tout le long du jour ils ont eu en mépris mes discours; toutes leurs pensées tendaient à me nuire.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
Ils s'établiront auprès de moi, s'embusqueront et guetteront mes pieds, comme ils ont cherché la perte de mon âme.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Tu ne les sauveras pas; tu briseras les peuples en ta colère, ô mon Dieu.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
Je t'ai dévoilé ma vie; tu as mis devant toi mes larmes, selon ta promesse.
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Mes ennemis tourneront le dos, quel que soit le jour où je t'invoque; voilà comment je reconnais que tu es mon Dieu.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
En Dieu je louerai la parole; en Dieu je louerai les discours.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
J'ai espéré en Dieu, je ne craindrai rien de ce que l'homme fera contre moi.
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
En moi sont les vœux de louange que je te rendrai, ô Dieu.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Car tu as délivré mon âme de la mort et mes pieds de la chute, afin que je sois agréable aux yeux de Dieu dans la lumière des vivants.

< Zaburi 56 >