< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
Au chef de musique. Sur Jonath-Élem-Rekhokim. De David. Mictam; quand les Philistins le prirent dans Gath. Use de grâce envers moi, ô Dieu! car l’homme voudrait m’engloutir; me faisant la guerre tout le jour, il m’opprime.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Mes ennemis voudraient tout le jour m’engloutir; car il y en a beaucoup qui me font la guerre, avec hauteur.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
Au jour où je craindrai, je me confierai en toi.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
En Dieu, je louerai sa parole; en Dieu je me confie: je ne craindrai pas; que me fera la chair?
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
Tout le jour ils tordent mes paroles; toutes leurs pensées sont contre moi en mal.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
Ils s’assemblent, ils se cachent, ils observent mes pas, car ils guettent mon âme.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Échapperont-ils par l’iniquité? Dans ta colère, ô Dieu, précipite les peuples!
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
Tu comptes mes allées et mes venues; mets mes larmes dans tes vaisseaux; ne sont-elles pas dans ton livre?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Alors mes ennemis retourneront en arrière, au jour où je crierai; je sais cela, car Dieu est pour moi.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
En Dieu, je louerai sa parole; en l’Éternel, je louerai sa parole.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
En Dieu je me confie: je ne craindrai pas; que me fera l’homme?
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
Les vœux que je t’ai faits sont sur moi, ô Dieu! je te rendrai des louanges.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Car tu as délivré mon âme de la mort: [ne garderais-tu] pas mes pieds de broncher, pour que je marche devant Dieu dans la lumière des vivants?

< Zaburi 56 >