< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
Pour le chef musicien. Sur l'air de « Silent Dove in Distant Lands ». Un poème de David, quand les Philistins l'ont saisi à Gath. Aie pitié de moi, Dieu, car l'homme veut m'engloutir. Toute la journée, il m'attaque et m'opprime.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Mes ennemis veulent m'engloutir toute la journée, car ils sont nombreux à se battre fièrement contre moi.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
Quand j'ai peur, Je vous fais confiance.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
En Dieu, je loue sa parole. En Dieu, je mets ma confiance. Je n'aurai pas peur. Que peut me faire la chair?
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
Tout le jour, ils déforment mes paroles. Toutes leurs pensées sont contre moi, pour le mal.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
Ils conspirent et se cachent, à regarder mes pas. Ils sont impatients de prendre ma vie.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Echapperont-ils par l'iniquité? Dans ta colère, renverse les peuples, Dieu.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
Tu comptes mes pérégrinations. Tu as mis mes larmes dans ton récipient. Ils ne sont pas dans votre livre?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Alors mes ennemis reculeront au jour où j'appellerai. Je sais ceci: que Dieu est pour moi.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
En Dieu, je louerai sa parole. En Yahvé, je louerai sa parole.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
J'ai mis ma confiance en Dieu. Je n'aurai pas peur. Que peut me faire l'homme?
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
Tes vœux sont sur moi, Dieu. Je vous donnerai des offrandes de remerciement.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Car tu as délivré mon âme de la mort, et empêchait mes pieds de tomber, afin que je puisse marcher devant Dieu dans la lumière des vivants.

< Zaburi 56 >