< Zaburi 56 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
To the Overseer. — 'On the Dumb Dove far off.' — A secret treasure of David, in the Philistines' taking hold of him in Gath. Favour me, O God, for man swallowed me up, All the day fighting he oppresseth me,
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Mine enemies have swallowed up all the day, For many [are] fighting against me, O most High,
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
The day I am afraid I am confident toward Thee.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
In God I praise His word, in God I have trusted, I fear not what flesh doth to me.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
All the day they wrest my words, Concerning me all their thoughts [are] for evil,
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
They assemble, they hide, they watch my heels, When they have expected my soul.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
By iniquity they escape, In anger the peoples put down, O God.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
My wandering Thou hast counted, Thou — place Thou my tear in Thy bottle, Are they not in Thy book?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Then turn back do mine enemies in the day I call. This I have known, that God [is] for me.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
In God I praise the word, In Jehovah I praise the word.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
In God I trusted, I fear not what man doth to me,
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
On me, O God, [are] Thy vows, I repay thank-offerings to Thee.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
For Thou hast delivered my soul from death, Dost Thou not my feet from falling? To walk habitually before God in the light of the living!