< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
`In Ebreu thus, To the ouercomyng on the doumb culuer of fer drawing awei, the comely song of Dauid, whanne Filisteis helden hym in Geth. `In Jeroms translacioun thus, To the ouercomer for the doumb culuer, for it yede awei fer. Dauid meke and symple made this salm, whanne Palesteyns helden hym in Geth. God, haue thou merci on me, for a man hath defoulid me; al dai he impugnyde, and troublide me.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Myn enemyes defouliden me al dai; for manye fiyteris weren ayens me.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
Of the hiynesse of dai Y schal drede; but God Y schal hope in thee.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
In God Y schal preise my wordis; Y hopide in God, Y schal not drede what thing fleisch schal do to me.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
Al dai thei cursiden my wordis; ayens me alle her thouytis weren in to yuel.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
Thei schulen dwelle, and schulen hide; thei schulen aspie myn heele.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
As thei abiden my lijf, for nouyt schalt thou make hem saaf; in ire thou schalt breke togidre puplis.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
God, Y schewide my lijf to thee; thou hast set my teeris in thi siyt. As and in thi biheest, Lord;
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
thanne myn enemyes schulen be turned abak. In what euere dai Y schal inwardli clepe thee; lo! Y haue knowe, that thou art my God.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
In God Y schal preise a word; in the Lord Y schal preyse a word.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
Y schal hope in God; Y schal not drede what thing a man schal do to me.
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
God, thin auowis ben in me; whiche Y schal yelde heriyngis to thee.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
For thou hast delyuerid my lijf fro deth, and my feet fro slidyng; that Y pleese bifore God in the liyt of hem that lyuen.

< Zaburi 56 >