< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
To the Chief Musician. Upon "The Dove of God from the distant Sea." David’s. A precious Psalm. When the Philistines seized him in Gath. Show me favour, O God, For weak man hath panted for me, All the day, a fighter oppresseth me:
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Mine adversaries have panted all the day, For, many, are fighting with me, loftily.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
What day I am afraid, I, unto thee will direct my confidence.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
In God, I will praise his cause, —In God, have I trusted, I will not fear, What can flesh do unto me?
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
All the day, they wrest, my words, Against me, all their devices are for mischief;
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
They stir up strife—they lie hid, They, mark my steps, —Seeing they have waited for my life.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Because of iniquity, recompense thou them, —In anger, bring thou down, the peoples, O God.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
My wandering, hast, thou, recorded, —Put thou my tears in thy bottle, Are they not in thy record?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Then, shall my foes turn back, in the day I cry, This, I know, for God is mine!
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
In God, will I praise with good cause: In Yahweh, will I praise with good cause;
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
In God, have I trusted, I will not fear, What can a son of earth do unto me!
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
Upon me, O God, are thy vows, I will pay back praises unto thee.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
For thou hast rescued my soul from death, Wilt thou not [rescue] my feet from stumbling? That I may walk to and fro, before God, In the light of life.

< Zaburi 56 >