< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
Unto the end, for a people that is removed at a distance from the sanctuary for David, for an inscription of a title (or pillar) when the Philistines held him in Geth. Have mercy on me, O God, for man hath trodden me under foot; all the day long he hath afflicted me fighting against me.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
My enemies have trodden on me all the day long; for they are many that make war against me.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
From the height of the day I shall fear: but I will trust in thee.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
In God I will praise my words, in God I have put my trust: I will not fear what flesh can do against me.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
All the day long they detested my words: all their thoughts were against me unto evil.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
They will dwell and hide themselves: they will watch my heel. As they have waited for my soul,
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
For nothing shalt thou save them: in thy anger thou shalt break the people in pieces, O God,
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
I have declared to thee my life: thou hast set my tears in thy sight, As also in thy promise.
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Then shall my enemies be turned back. In what day soever I shall call upon thee, behold I know thou art my God.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
In God will I praise the word, in the Lord will I praise his speech.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
In God have I hoped, I will not fear what man can do to me.
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
In me, O God, are vows to thee, which I will pay, praises to thee:
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
Because thou hast delivered my soul from death, my feet from falling: that I may please in the sight of God, in the light of the living.

< Zaburi 56 >