< Zaburi 56 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
For the end, concerning the people that were removed from the sanctuary, by David for a memorial, when the Philistines caught him in Geth. Have mercy upon me, O God; for man has trodden me down; all the day long he warring has afflicted me.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
Mine enemies have trodden me down all the day from the dawning of the day; for there are many warring against me.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
They shall be afraid, but I will trust in thee.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
In God I will praise my words; all the day have I hoped in God; I will not fear what flesh shall do to me.
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
All the day long they have abominated my words; all their devices [are] against me for evil.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
They will dwell near and hide [themselves]; they will watch my steps, accordingly as I have waited patiently in my soul.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Thou wilt on no account save them; thou wilt bring down the people in wrath.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
O God, I have declared my life to thee; thou has set my tears before thee, even according to thy promise.
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Mine enemies shall be turned back, in the day wherein I shall call upon thee; behold, I know that thou art my God.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
In God, will I praise [his] word; in the Lord will I praise [his] saying.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
I have hoped in God; I will not be afraid of what man shall do to me.
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
The vows of thy praise, O God, which I will pay, are upon me.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
For thou hast delivered my soul from death, and my feet from sliding, that I should be well-pleasing before God in the land of the living.