< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
非利士人在迦特拿住大卫。那时,他作这金诗,交与伶长。调用远方无声鸽。 神啊,求你怜悯我,因为人要把我吞了, 终日攻击欺压我。
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
我的仇敌终日要把我吞了, 因逞骄傲攻击我的人甚多。
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
我惧怕的时候要倚靠你。
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
我倚靠 神,我要赞美他的话; 我倚靠 神,必不惧怕。 血气之辈能把我怎么样呢?
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
他们终日颠倒我的话; 他们一切的心思都是要害我。
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
他们聚集,埋伏窥探我的脚踪, 等候要害我的命。
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
他们岂能因罪孽逃脱吗? 神啊,求你在怒中使众民堕落!
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
我几次流离,你都记数; 求你把我眼泪装在你的皮袋里。 这不都记在你册子上吗?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
我呼求的日子,我的仇敌都要转身退后。 神帮助我,这是我所知道的。
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
我倚靠 神,我要赞美他的话; 我倚靠耶和华,我要赞美他的话。
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
我倚靠 神,必不惧怕。 人能把我怎么样呢?
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
神啊,我向你所许的愿在我身上; 我要将感谢祭献给你。
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
因为你救我的命脱离死亡。 你岂不是救护我的脚不跌倒、 使我在生命光中行在 神面前吗?

< Zaburi 56 >