< Zaburi 54 >

1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
MAIN Kot, kom kotin jauaj a ia ki mar omui, o kotin kajanjaleda ai pun ki omui manaman.
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
Main Kot, kom kotin ereki ai kapakap, o kotin mani lokaia en au i.
3 Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
Pwe men wai kai palian ia, o me weit akan majamajan maur i, o re jota weweid mon Kot.
4 Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
Kilan, Kot jauaj pa i, leowa kin kolekol nen i.
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
A pan kotin depuk on ai imwintiti kan ar me jued. Kom kotin kawe ir ala ki omui melel.
6 Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
I ap pan wiai on komui mairon kaperen, o kapina mar omui, pwe a me mau.
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
Pwe a kotin dore ia la jan nan ai apwal akan karoj, o maj ai peren kidar ai imwintiti kan.

< Zaburi 54 >