< Zaburi 54 >

1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
למנצח בנגינת משכיל לדוד בבוא הזיפים ויאמרו לשאול הלא דוד מסתתר עמנו אלהים בשמך הושיעני ובגבורתך תדינני׃
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
אלהים שמע תפלתי האזינה לאמרי פי׃
3 Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
כי זרים קמו עלי ועריצים בקשו נפשי לא שמו אלהים לנגדם סלה׃
4 Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
הנה אלהים עזר לי אדני בסמכי נפשי׃
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
ישוב הרע לשררי באמתך הצמיתם׃
6 Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
בנדבה אזבחה לך אודה שמך יהוה כי טוב׃
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
כי מכל צרה הצילני ובאיבי ראתה עיני׃

< Zaburi 54 >