< Zaburi 54 >
1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
For the leader. With stringed instruments. A maskil of David, when the Ziphites came and said to Saul, “David is in hiding among us”. Save me, O God, by your name, by your power secure for me justice.
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
Listen, O God, to my prayer, attend to the words of my mouth.
3 Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
For proud men have risen against me, and terrible men seek my life, men who do not set God before them. (Selah)
4 Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
But see! God is my helper, the Lord is sustaining my life.
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
Let their evil fall back on my foes: cut them off in your faithfulness, Lord.
6 Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
Then will I bring you glad sacrifice, praising your gracious name;
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
for from all distress you have saved me, and feasted my eyes on my foes.