< Zaburi 54 >
1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
For the end, among Hymns of instruction by David, when the Ziphites came and said to Saul, Lo, is not David hid with us? Save me, O God, by thy name, and judge me by thy might.
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
O God, hear my prayer; hearken to the words of my mouth.
3 Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
For strangers have risen up against me, and mighty men have sought my life: they have not set God before them. (Pause)
4 Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
For lo! God assists me; and the Lord is the helper of my soul.
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
He shall return evil to mine enemies; utterly destroy them in thy truth.
6 Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
I will willingly sacrifice to thee: I will give thanks to thy name, O Lord; for [it is] good.
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
For thou hast delivered me out of all affliction, and mine eye has seen [my desire] upon mine enemies.