< Zaburi 54 >
1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
For the choirmaster. With stringed instruments. A Maskil of David. When the Ziphites went to Saul and said, “Is David not hiding among us?” Save me, O God, by Your name, and vindicate me by Your might!
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
Hear my prayer, O God; listen to the words of my mouth.
3 Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
For strangers rise up against me, and ruthless men seek my life— men with no regard for God.
4 Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
Surely God is my helper; the Lord is the sustainer of my soul.
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
He will reward my enemies with evil. In Your faithfulness, destroy them.
6 Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
Freely I will sacrifice to You; I will praise Your name, O LORD, for it is good.
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
For He has delivered me from every trouble, and my eyes have stared down my foes.