< Zaburi 54 >

1 Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
西弗人來對掃羅說:「大衛豈不是在我們那裏藏身嗎?」那時,大衛作這訓誨詩,交與伶長。用絲弦的樂器。 上帝啊,求你以你的名救我, 憑你的大能為我伸冤。
2 Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
上帝啊,求你聽我的禱告, 留心聽我口中的言語。
3 Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
因為,外人起來攻擊我, 強暴人尋索我的命; 他們眼中沒有上帝。 (細拉)
4 Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
上帝是幫助我的,是扶持我命的。
5 Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
他要報應我仇敵所行的惡; 求你憑你的誠實滅絕他們。
6 Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
我要把甘心祭獻給你。 耶和華啊,我要稱讚你的名;這名本為美好。
7 Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.
他從一切的急難中把我救出來; 我的眼睛也看見了我仇敵遭報。

< Zaburi 54 >