< Zaburi 53 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
Para el director del coro. Según Mahalat. Un salmo (masquil) de David. Solo los tontos se dicen a sí mismos, “Dios no existe”. Son completamente inmorales, cometen pecados terribles, ni uno solo de ellos hace algo bueno.
2 Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
Dios observa desde los cielos para ver si alguien entiende, si alguien quiere venir a él.
3 Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
Todos han caído, son totalmente depravados; ninguno hace el bien, ni siquiera uno.
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
“¿Nunca aprenderá este pueblo que hace el mal? Consumen a mi pueblo como si estuvieran comiendo pan, y se niegan a invocar mi nombre”.
5 Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
Se aterrorizarán por completo, tendrán más miedo del que nunca han tenido. Dios esparcirá los huesos de los que pelean contra ti; los derrotarás porque Dios los ha rechazado.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
¡Si tan solo la salvación de Dios viniera de Sión! Cuando Dios restaure a su pueblo, el pueblo de Jacob celebrará, y el pueblo de Israel se alegrará.