< Zaburi 53 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
Au maître-chantre. — Sur un mode triste. — Hymne de David. L'insensé a dit en son coeur: «Il n'y a point de Dieu!» Les hommes sont corrompus: leur conduite est abominable; Il n'y a personne qui fasse le bien.
2 Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
Dieu abaisse des cieux son regard sur les fils des hommes, Pour voir s'il y a quelque homme intelligent Et qui cherche Dieu.
3 Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
Ils se sont tous égarés, ils se sont pervertis tous ensemble: Il n'y en a pas qui fasse le bien. Non, pas même un seul!
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
Sont-ils donc sans intelligence, ces ouvriers d'iniquité? Ils dévorent mon peuple comme on mange du pain; Ils n'invoquent point Dieu!
5 Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
Ils seront saisis d'une terreur soudaine. Sans avoir aucun sujet de crainte; Car Dieu dispersera les os de ceux qui t'assiègent. Tu les couvriras de honte; car Dieu les a rejetés.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
Oh! Qui apportera de Sion la délivrance d'Israël? Quand Dieu ramènera les captifs de son peuple, Jacob sera dans l'allégresse, Israël sera dans la joie.

< Zaburi 53 >