< Zaburi 53 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
To the ouercomer bi the quere, the lernyng of Dauid. The vnwise man seide in his herte; God is not. Thei ben `corrupt, and maad abhomynable in her wickidnessis; noon is that doith good.
2 Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
God bihelde fro heuene on the sones of men; that he se, if `ony is vndurstondynge, ether sekynge God.
3 Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
Alle boweden awei, thei ben maad vnprofitable togidre; noon is that doith good, ther is not til to oon.
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
Whether alle men, that worchen wickidnesse, schulen not wite; whiche deuouren my puple as the mete of breed?
5 Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
Thei clepiden not God; there thei trembliden for drede, where no drede was. For God hath scaterid the boones of hem, that plesen men; thei ben schent, for God hath forsake hem.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
Who schal yyue fro Syon helthe to Israel? whanne the Lord hath turned the caitifte of his puple, Jacob schal `ful out make ioie, and Israel schal be glad.

< Zaburi 53 >