< Zaburi 53 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
to/for to conduct upon Mahalath Maskil to/for David to say foolish in/on/with heart his nothing God to ruin and to abhor injustice nothing to make: do good
2 Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
God from heaven to look upon son: child man to/for to see: see there be prudent to seek [obj] God
3 Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
all his to turn together to corrupt nothing to make: do good nothing also one
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
not to know to work evil: wickedness to eat people my to eat food: bread God not to call: call to
5 Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
there to dread dread not to be dread for God to scatter bone to camp you be ashamed for God to reject them
6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
who? to give: if only! from Zion salvation Israel in/on/with to return: rescue God captivity people his to rejoice Jacob to rejoice Israel

< Zaburi 53 >