< Zaburi 53 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
For the Leader; upon Mahalath. Maschil of David. The fool hath said in his heart: 'There is no God'; they have dealt corruptly, and have done abominable iniquity; there is none that doeth good.
2 Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
God looked forth from heaven upon the children of men, to see if there were any man of understanding, that did seek after God.
3 Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
Every one of them is unclean, they are together become impure; there is none that doeth good, no, not one.
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
'Shall not the workers of iniquity know it, who eat up My people as they eat bread, and call not upon God?'
5 Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
There are they in great fear, where no fear was; for God hath scattered the bones of him that encampeth against thee; Thou hast put them to shame, because God hath rejected them.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
Oh that the salvation of Israel were come out of Zion! When God turneth the captivity of His people, let Jacob rejoice, let Israel be glad.

< Zaburi 53 >