< Zaburi 52 >

1 Kwa mwimbishaji. Utenzi wa Daudi. Baada ya Doegi, Mwedomu kumwendea Sauli na kumjulisha kuwa: “Daudi amekwenda nyumbani kwa Ahimeleki.” Ewe jitu, mbona unajivunia ubaya? Kwa nini unajivuna mchana kutwa, wewe ambaye ni fedheha mbele za Mungu?
למנצח משכיל לדוד בבוא דואג האדמי ויגד לשאול ויאמר לו בא דוד אל בית אחימלך מה תתהלל ברעה הגבור חסד אל כל היום׃
2 Ulimi wako hupanga mashauri mabaya ya maangamizi. Ni kama wembe mkali, ninyi mfanyao hila.
הוות תחשב לשונך כתער מלטש עשה רמיה׃
3 Unapenda mabaya kuliko mema, uongo kuliko kusema kweli.
אהבת רע מטוב שקר מדבר צדק סלה׃
4 Unapenda kila neno lenye kudhuru, ewe ulimi wenye hila!
אהבת כל דברי בלע לשון מרמה׃
5 Hakika Mungu atakushusha chini kwa maangamizi ya milele: atakunyakua na kukuondoa kwa nguvu kutoka hema yako, atakungʼoa kutoka nchi ya walio hai.
גם אל יתצך לנצח יחתך ויסחך מאהל ושרשך מארץ חיים סלה׃
6 Wenye haki wataona na kuogopa, watamcheka, wakisema,
ויראו צדיקים וייראו ועליו ישחקו׃
7 “Huyu ni yule mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa ngome yake, bali alitumainia wingi wa utajiri wake, na akawa hodari kwa kuwaangamiza wengine!”
הנה הגבר לא ישים אלהים מעוזו ויבטח ברב עשרו יעז בהותו׃
8 Lakini mimi ni kama mti wa mzeituni unaostawi katika nyumba ya Mungu, nautegemea upendo wa Mungu usiokoma milele na milele.
ואני כזית רענן בבית אלהים בטחתי בחסד אלהים עולם ועד׃
9 Nitakusifu milele kwa yale uliyoyatenda, nitatumaini jina lako, kwa kuwa jina lako ni jema. Nitakusifu mbele ya watakatifu wako.
אודך לעולם כי עשית ואקוה שמך כי טוב נגד חסידיך׃

< Zaburi 52 >