< Zaburi 51 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba. Ee Mungu, unihurumie, kwa kadiri ya upendo wako usiokoma, kwa kadiri ya huruma yako kuu, uyafute makosa yangu.
ダビデがバテセバにかよひしのち預言者ナタンの來れるときよみて伶長にうたはしめたる歌 ああ神よねがはくはなんぢの仁慈によりて我をあはれみ なんぢの憐憫のおほきによりてわがもろもろの愆をけしたまへ
2 Unioshe na uovu wangu wote na unitakase dhambi yangu.
わが不義をことごとくあらひさり我をわが罪よりきよめたまへ
3 Kwa maana ninajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
われはわが愆をしる わが罪はつねにわが前にあり
4 Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi na kufanya yaliyo mabaya machoni pako, ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo, na kuwa na haki utoapo hukumu.
我はなんぢにむかひて獨なんぢに罪ををかし聖前にあしきことを行へり されば汝ものいふときは義とせられ なんぢ鞫くときは咎めなしとせられ給ふ
5 Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi, mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
視よわれ邪曲のなかにうまれ罪ありてわが母われをはらみたりき
6 Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni, ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.
なんぢ眞実をこころの衷にまでのぞみ わが隠れたるところに智慧をしらしめ給はん
7 Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi, unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
なんぢヒソブをもて我をきよめたまへ さらばわれ浄まらん 我をあらひたまへ さらばわれ雪よりも白からん
8 Unipe kusikia furaha na shangwe, mifupa uliyoiponda na ifurahi.
なんぢ我によろこびと快樂とをきかせ なんぢが砕きし骨をよろこばせたまへ
9 Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu, na uufute uovu wangu wote.
ねがはくは聖顔をわがすべての罪よりそむけ わがすべての不義をけしたまへ
10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.
ああ神よわがために清心をつくり わが衷になほき霊をあらたにおこしたまへ
11 Usinitupe kutoka mbele zako wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.
われを聖前より棄たまふなかれ 汝のきよき霊をわれより取りたまふなかれ
12 Unirudishie tena furaha ya wokovu wako, unipe roho ya utii, ili initegemeze.
なんぢの救のよろこびを我にかへし自由の霊をあたへて我をたもちたまへ
13 Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
さらばわれ愆ををかせる者になんぢの途ををしへん罪人はなんぢに婦りきたるべし
14 Ee Mungu, Mungu uniokoaye, niokoe na hatia ya kumwaga damu, nao ulimi wangu utaimba juu ya haki yako.
神よわが救のかみよ血をながしし罪より我をたすけいだしたまへ わが舌は聲たからかになんぢの義をうたはん
15 Ee Bwana, fungua midomo yangu, na kinywa changu kitatangaza sifa zako.
主よわが口唇をひらきたまへ 然ばわが口なんぢの頌美をあらはさん
16 Wewe hupendezwi na dhabihu, au ningaliileta, hufurahii sadaka za kuteketezwa.
なんぢは祭物をこのみたまはず もし然らずば我これをささげん なんぢまた燔祭をも悦びたまはず
17 Bali dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika, moyo uliovunjika wenye toba, Ee Mungu, hutaudharau.
神のもとめたまふ祭物はくだけたる霊魂なり 神よなんぢは砕けたる悔しこころを藐しめたまふまじ
18 Kwa wema wa radhi yako uifanye Sayuni istawi, ukazijenge upya kuta za Yerusalemu.
ねがはくは聖意にしたがひてシオンにさいはひし ヱルサレムの石垣をきづきたまへ
19 Hapo ndipo kutakapokuwa na dhabihu za haki, sadaka nzima za kuteketezwa za kukupendeza sana, pia mafahali watatolewa madhabahuni mwako.
その時なんぢ義のそなへものと燔祭と全きはんさいとを悦びたまはん かくて人汝なんぢの祭壇に牡牛をささぐべし