< Zaburi 50 >
1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
El Dios de los dioses, el Señor, ha enviado su voz, y la tierra está llena de temor; desde la llegada del sol hasta su descenso.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Desde Sión, el más bello de los lugares, Dios ha enviado su luz.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Nuestro Dios vendrá, y no callará; con fuego ardiendo delante de él y vientos de tormenta a su alrededor.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Convocará los cielos y a la tierra para juzgar a su pueblo.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Dejen que mis santos se reúnan conmigo; aquellos que han hecho un acuerdo conmigo por medio de ofrendas.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Y los cielos declaran su justicia; porque Dios mismo es el juez. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Escucha, pueblo mío, a mis palabras; Oh Israel, seré testigo contra ti; Yo soy Dios, tu Dios.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
No tomaré una causa contra ti por tus ofrendas, ni por tus ofrendas quemadas, que están siempre ante mí.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
No tomaré buey de tu casa, ni macho cabríos de tus corrales;
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Porque toda bestia del bosque es mía, y el ganado en mil colinas.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Veo todas las aves de los montes, y las bestias del campo son mías.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Si tuviera necesidad de comida, no te diría a ti; porque la tierra es mía y toda su plenitud.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
¿Debo tomar la carne del buey para mi alimento, o la sangre de las cabras para mi bebida?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Haz una ofrenda de alabanza a Dios; mantén los acuerdos que has hecho con el Altísimo;
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Invócame en el día de la angustia; Seré tu salvador, para que puedas darme gloria.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Pero al pecador, Dios le dice: ¿Qué estás haciendo, hablando de mis leyes, o tomando las palabras de mi acuerdo en tu boca?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Al ver que no tienes ningún deseo de mi enseñanza, y le das la espalda a mis palabras.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Cuando viste a un ladrón, estabas de acuerdo con él, y te uniste con los adúlteros.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Usas tu boca para mal, tu lengua a las palabras del engaño.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Dices mal de tu hermano; haces declaraciones falsas contra el hijo de tu madre.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Estas cosas has hecho, y yo no he dicho nada; te pareció que yo era uno como tú; pero te reprenderé cara a cara y voy ajustarte las cuentas.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Ahora ten esto en mente, tú que no tienes memoria de Dios, por temor a que seas aplastado bajo mi mano, sin nadie para darte ayuda:
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
El que hace una ofrenda de alabanza me glorifica; y al que es recto en sus caminos, le mostraré la salvación de Dios.