< Zaburi 50 >
1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Salmo de Asaph. EL Dios de dioses, Jehová, ha hablado, y convocado la tierra desde el nacimiento del sol hasta donde se pone.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
De Sión, perfección de hermosura, ha Dios resplandecido.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Vendrá nuestro Dios, y no callará: fuego consumirá delante de él, y en derredor suyo habrá tempestad grande.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Convocará á los cielos de arriba, y á la tierra, para juzgar á su pueblo.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Juntadme mis santos; los que hicieron conmigo pacto con sacrificio.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Y denunciarán los cielos su justicia; porque Dios es el juez. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Oye, pueblo mío, y hablaré: [escucha], Israel, y testificaré contra ti: yo soy Dios, el Dios tuyo.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
No te reprenderé sobre tus sacrificios, ni por tus holocaustos, que delante de mí están siempre.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
No tomaré de tu casa becerros, ni machos cabríos de tus apriscos.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Porque mía es toda bestia del bosque, y los millares de animales en los collados.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Conozco todas las aves de los montes, y en mi poder están las fieras del campo.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Si yo tuviese hambre, no te lo diría á ti: porque mío es el mundo y su plenitud.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
¿Tengo de comer yo carne de toros, ó de beber sangre de machos cabríos?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Sacrifica á Dios alabanza, y paga tus votos al Altísimo.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
E invócame en el día de la angustia: te libraré, y tú me honrarás.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Pero al malo dijo Dios: ¿Qué tienes tú que enarrar mis leyes, y que tomar mi pacto en tu boca,
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Pues que tú aborreces el castigo, y echas á tu espalda mis palabras?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Si veías al ladrón, tú corrías con él; y con los adúlteros era tu parte.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Tu boca metías en mal, y tu lengua componía engaño.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Tomabas asiento, [y] hablabas contra tu hermano; contra el hijo de tu madre ponías infamia.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Estas cosas hiciste, y yo he callado: pensabas que de cierto sería yo como tú: yo te argüiré, y pondré[las] delante de tus ojos.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Entended ahora esto, los que os olvidáis de Dios; no sea que arrebate, sin que nadie libre.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
El que sacrifica alabanza me honrará: y al que ordenare su camino, le mostraré la salud de Dios.