< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Psalm Asafu; Bog mogočni, Bog Gospod govori in kliče zemljo od vzhoda solnčnega do zahoda.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Sè Sijona, najvišje lepote, proseva Bog.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
(Pridi, naš Bog, in ne delaj se gluhega); ogenj razsaja pred njim, in silno viharno je okrog njega.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Nebesa kliče od zgoraj, in zemljo, da sodi ljudstvo svoje:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Zberite mi jih, katerim sem delil milost, kateri so storili zavezo z menoj po daritvi.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Ko so nebesa oznanjala pravico njegovo, da je Bog sodnik,
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Čuj, ljudstvo moje, in govoril bodem, Izrael, in na pričo te klical; Bog, Bog naj bodem tvoj.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Ne zavoljo daritev tvojih te bodem svaril, da naj bodejo žgalne daritve tvoje vedno pred menoj.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Ne sprejmem iz hiše tvoje junca, kozličev iz tvojih ograj.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Ker moja je vsaka gozdna zver, živali v gorah tisoč,
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Vse tiče gorske poznam, in živali poljske so v moji oblasti.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Ko bi bil gladen, ne rekel bi tebi; ker moja je zemlja vesoljna in njena obilost.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Ali živim o mesu krepkih juncev, ali pijem kozlov kri?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Hvalo daruj Bogu, in najvišjemu opravljaj obljube svoje.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
In kliči me o času stiske; rešil te bodem, da me čestiš.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Krivičnemu pa pravi Bog: Kaj da naštevaš zapovedi moje in jemlješ zavezo mojo v svoja usta?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Ker ti sovražiš poštenje, in besede moje si vrgel zá se.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Kakor hitro vidiš tatú, sprijazniš se z njim; in s prešestniki je delež tvoj.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Usta svoja rabiš za húdo, in z jezikom svojim spletaš zvijačo.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Sedé obrekuješ svojega brata, sina matere svoje sramotiš.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Ko si to počel, delal sem se gluhega; zato meniš, da sem prav tebi podoben: svarim te in govorim ti v óči.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Pázite vendar na to vi, ki zábite Boga, da ne zgrabim in ga ne bode, da bi rešil.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Kdor daruje hvalo, česti me, in kdor uravnava pot, storil bodem, da uživa blaginjo Božjo.

< Zaburi 50 >