< Zaburi 50 >
1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Asafa dziesma. Tas stiprais Dievs, Dievs Tas Kungs, runā, un sauc zemi no rītiem līdz vakariem.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
No Ciānas, kur tas pilnīgais skaistums, Dievs parādās ar spožumu.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Mūsu Dievs nāk un necieš klusu; rijoša uguns iet Viņa priekšā, un Viņam apkārt liela vētra.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Viņš sauc debesīm augšā, un zemei, tiesāt Savus ļaudis.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Sapulcinājiet Man Manus svētos, kas Manu derību derējuši ar upuriem.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Un debesis stāsta Viņa taisnību, jo Dievs pats ir soģis. (Sela)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Klausiet, Mani ļaudis, Es runāšu; Israēl, Es došu liecību pret tevi: Es, Dievs, esmu tavs Dievs.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Tavu upuru pēc Es tevi nepārmācu, nedz tavu dedzināmo upuru pēc, kas vienmēr Manā priekšā.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
No tava nama Es vēršus neņemšu, nedz āžus no taviem laidariem.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Jo visi meža zvēri Man pieder, tie lopi uz kalniem pa tūkstošiem.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Es zinu visus putnus uz kalniem, un tie zvēri laukā ir manā priekšā.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Ja Man gribētos ēst, tad Es tev to nesacītu, jo Man pieder pasaule un viņas pilnums.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Vai Man ēst vērša gaļu un dzert āžu asinis?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Upurē Dievam pateicību un maksā tam Visuaugstam savus solījumus.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Un piesauc Mani bēdu laikā, tad Es tevi gribu izraut, un tev būs Mani godāt.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Bet uz bezdievīgo Dievs saka: kā tu drīksti daudzināt Manus likumus un Manu derību ņemt savā mutē.
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Kad tu tomēr ienīsti pārmācību, un laidi pār galvu Manus vārdus?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Kad tu zagli redzi, tad tu viņam skrej līdz, un tev ir dalība ar laulības pārkāpējiem.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Ar savu muti tu dodies uz ļaunu, un tava mēle dzen viltību.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Tu sēdi runādams pret savu brāli, tavas mātes dēlu tu apmelo.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
To tu dari, un kad Es ciešu klusu, tad tu domā, ka Es tāds pat esmu kā tu; bet Es tevi pārmācīšu un tev to turēšu priekš acīm.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Saprotiet jel to, jūs, kas Dievu aizmirstat, lai Es nesaplosu, un izglābēja nav.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Kas pateicību upurē, tas Mani tur godā; un tas ir tas ceļš, kā Es tam rādīšu Dieva pestīšanu.