< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
מזמור לאסף אל אלהים יהוה דבר ויקרא ארץ ממזרח שמש עד מבאו׃
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
מציון מכלל יפי אלהים הופיע׃
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
יבא אלהינו ואל יחרש אש לפניו תאכל וסביביו נשערה מאד׃
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
יקרא אל השמים מעל ואל הארץ לדין עמו׃
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
אספו לי חסידי כרתי בריתי עלי זבח׃
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
ויגידו שמים צדקו כי אלהים שפט הוא סלה׃
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
שמעה עמי ואדברה ישראל ואעידה בך אלהים אלהיך אנכי׃
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
לא על זבחיך אוכיחך ועולתיך לנגדי תמיד׃
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
לא אקח מביתך פר ממכלאתיך עתודים׃
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
כי לי כל חיתו יער בהמות בהררי אלף׃
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
ידעתי כל עוף הרים וזיז שדי עמדי׃
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
אם ארעב לא אמר לך כי לי תבל ומלאה׃
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
האוכל בשר אבירים ודם עתודים אשתה׃
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
זבח לאלהים תודה ושלם לעליון נדריך׃
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
וקראני ביום צרה אחלצך ותכבדני׃
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
ולרשע אמר אלהים מה לך לספר חקי ותשא בריתי עלי פיך׃
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
ואתה שנאת מוסר ותשלך דברי אחריך׃
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
אם ראית גנב ותרץ עמו ועם מנאפים חלקך׃
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
פיך שלחת ברעה ולשונך תצמיד מרמה׃
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
תשב באחיך תדבר בבן אמך תתן דפי׃
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
אלה עשית והחרשתי דמית היות אהיה כמוך אוכיחך ואערכה לעיניך׃
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
בינו נא זאת שכחי אלוה פן אטרף ואין מציל׃
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
זבח תודה יכבדנני ושם דרך אראנו בישע אלהים׃

< Zaburi 50 >