< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Psaume d’Asaph.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
C’est de Sion que vient l’éclat de sa splendeur.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Dieu viendra manifestement: notre Dieu viendra, et il ne gardera pas le silence.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
D’en haut il appellera le ciel et la terre pour juger son peuple.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Rassemblez-lui ses saints, qui exécutent son alliance sur les sacrifices.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Et les cieux annonceront sa justice, parce que c’est Dieu lui-même qui est juge.
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Écoute, mon peuple, et je parlerai; Israël, écoute; car je te prendrai à témoin: Dieu, ton Dieu, c’est moi qui le suis.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Je ne te reprendrai pas pour tes sacrifices; car tes holocaustes sont toujours en ma présence.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Je ne prendrai pas des veaux de ta maison, ni des boucs de tes troupeaux.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Parce qu’à moi sont toutes les bêtes des forêts, les animaux qui paissent sur les montagnes et les bœufs.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Je connais tous les volatiles du ciel, et la beauté des champs est en mon pouvoir.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Si j’ai faim, je ne te le dirai pas: car à moi est le globe de la terre, et sa plénitude.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Est-ce que je mangerai des chairs de taureaux? ou boirai-je du sang des boucs?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Immole à Dieu un sacrifice de louange, et rends au Très-Haut tes vœux.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Et invoque-moi, au jour de la tribulation: je te délivrerai, et tu m’honoreras.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Mais au pécheur Dieu a dit: Pourquoi racontes-tu mes justices, et pourquoi ta bouche annonce-t-elle mon alliance?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Pour toi, tu hais la discipline, et tu as rejeté ma parole derrière toi.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Si tu voyais un voleur, tu courais avec lui, et c’est avec les adultères que tu mettais ta part.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Ta bouche a abondé en malice, et ta langue ajustait des fourberies.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Assis, tu parlais contre ton frère et contre le fils de ta mère, tu posais une pierre d’achoppement.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Tu as fait ces choses, et je me suis tu.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Comprenez ces choses, vous qui oubliez Dieu; de peur qu’un jour il ne vous enlève, et qu’il n’y ait personne qui vous délivre.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
C’est un sacrifice de louange qui m’honorera; et c’est là le chemin par lequel je lui montrerai le salut de Dieu.

< Zaburi 50 >