< Zaburi 50 >
1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Psaume d'Asaph. Le Dieu des dieux, le Seigneur a parlé, et il a appelé la terre depuis l'Orient jusqu'à l'Occident
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
De Sion vient la splendeur de sa beauté.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Dieu, notre Dieu viendra manifestement, et ne gardera pas le silence; un feu sera allume en sa présence, et tout alentour un vent impétueux soufflera.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Il convoquera le ciel et la terre, pour juger son peuple.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Amenez-lui ses saints, ceux qui ont fait alliance avec lui, pour les sacrifices.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Et les cieux annonceront sa justice; car Dieu est le juge.
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Écoute, mon peuple, et je parlerai; Israël, je te l'atteste: je suis Dieu, je suis ton Dieu.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Je ne te réprimanderai point sur tes sacrifices; car tes holocaustes sont toujours devant mes yeux.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Je ne prendrai pas de bœufs de ta maison, ni de boucs de tes menus troupeaux.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Car toutes les bêtes de la forêt m'appartiennent, et le bétail des montagnes et les taureaux.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Je connais tous les oiseaux du ciel, et la beauté des champs est à moi.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Si j'ai faim, je ne te le dis pas; car toute la terre habitée m'appartient et sa plénitude.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Est-ce que je mange la chair des taureaux? est-ce que je bois le sang des boucs?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Immole à Dieu une victime de louanges; rends au Tout-Puissant tes vœux.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Invoque-moi au jour de l'affliction, et je te sauverai, et tu me rendras grâces.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Mais Dieu a dit au pécheur: Pourquoi publies-tu mes justices et as-tu mon alliance à la bouche,
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Quand tu n'aimes point ma discipline, et que tu as rejeté loin de toi ma parole?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Si tu voyais un larron, tu courais avec lui; tu avais ta part avec les adultères;
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Ta bouche abondait en méchanceté, et ta langue tramait la fraude.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Assis, tu médisais de ton frère; tu scandalisais le fils de ta mère.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Voilà ce que tu faisais, et j'ai gardé le silence; mais tu t'imaginais faussement que je serais semblable à toi. Je te convaincrai, et je mettrai tes offenses devant ta face.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Comprenez donc ces choses, vous qui oubliez Dieu; de peur qu'un jour il ne vous ravisse, et que nul ne vous délivre.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
C'est un sacrifice de louange qui m'honore, et la voie où je montrerai le salut de Dieu.