< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Psaume d’Assaph. Le Dieu tout-puissant, l’Eternel parle; il adresse un appel à la terre, du soleil levant jusqu’à son couchant.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
De Sion, ce centre de beauté, l’Eternel rayonne.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Il s’avance, notre Dieu, et ce n’est pas en silence: devant lui, un feu qui dévore, autour de lui gronde la tempête.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Il adresse son appel aux cieux d’en haut ainsi qu’à la terre, en vue de juger son peuple:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
"Rassemblez-moi mes pieux serviteurs, qui ont sanctionné mon alliance par un sacrifice!"
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Et les cieux proclament sa justice, car c’est Dieu qui est le juge. (Sélah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Ecoute, mon peuple, je veux parler; Israël, je veux t’adjurer solennellement: Je suis Dieu, ton Dieu!
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Ce n’est pas pour tes sacrifices que je te reprends: tes holocaustes sont constamment sous mes yeux.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Je ne réclame pas de taureau de ta maison, ni des béliers de tes parcs.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Car à moi sont tous les fauves de la forêt, les bêtes qui peuplent par milliers les montagnes.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Je connais tous les oiseaux des hauteurs, tout ce qui se meut dans les champs est à ma portée.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Dussé-je avoir faim, je ne te le dirais pas, car l’univers, avec ce qu’il renferme, m’appartient.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Est-ce donc que je mange la chair des taureaux? Est-ce que je bois le sang des béliers?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
En guise de sacrifice, offre à Dieu des actions de grâce, ainsi tu acquitteras tes vœux envers le Très-Haut.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Alors tu pourras m’appeler au jour de la détresse, je te tirerai du danger, et tu m’honoreras!
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Quant au méchant, Dieu lui dit: "Qu’as-tu à proclamer mes statuts et à porter mon alliance sur tes lèvres?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Tu détestes pourtant la loi morale, et rejettes avec dédain mes paroles.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Vois-tu un voleur? Tu fais cause commune avec lui, tu t’associes avec des gens dissolus.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Tu donnes libre carrière à ta bouche pour le mal, et ta langue enfile des discours astucieux.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Tu t’installes pour déblatérer contre ton frère; sur le fils de ta mère tu jettes le déshonneur.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Voilà ce que tu fais, et je me tairais! T’Imagines-tu que je puisse être comme toi? Je te reprendrai et te mettrai mes griefs sous les yeux."
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Faites-y donc attention, vous qui oubliez Dieu, de peur que je ne sévisse, sans que personne puisse détourner mes coups.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Quiconque offre comme sacrifice des actions de grâce m’honore; quiconque dirige avec soin sa conduite, je le ferai jouir de l’aide divine.

< Zaburi 50 >