< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Psaume d’Asaph. Le [Dieu] Fort, Dieu, l’Éternel, a parlé, et a appelé la terre, du soleil levant jusqu’au soleil couchant.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
De Sion, perfection de la beauté, Dieu a fait luire sa splendeur.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Notre Dieu viendra, et il ne se taira point; un feu dévorera devant lui, et autour de lui tourbillonnera la tempête;
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Il appellera les cieux d’en haut, et la terre, pour juger son peuple:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Assemblez-moi mes saints, qui ont fait alliance avec moi par [un] sacrifice.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Et les cieux déclareront sa justice, car Dieu lui-même est juge. (Sélah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Écoute, mon peuple, et je parlerai; [écoute], Israël, et je témoignerai au milieu de toi. Moi, je suis Dieu, ton Dieu.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Je ne te reprendrai pas à cause de tes sacrifices ou de tes holocaustes, qui ont été continuellement devant moi.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Je ne prendrai pas de taureau de ta maison, ni de boucs de tes parcs;
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Car tout animal de la forêt est à moi, les bêtes sur mille montagnes.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Je connais tous les oiseaux des montagnes, et ce qui se meut par les champs est à moi.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Si j’avais faim, je ne te le dirais pas; car le monde est à moi, et tout ce qu’il contient.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Mangerais-je la chair des gros taureaux, et boirais-je le sang des boucs?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Sacrifie à Dieu la louange, et acquitte tes vœux envers le Très-haut,
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Et invoque-moi au jour de la détresse: je te délivrerai, et tu me glorifieras.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Mais Dieu dit au méchant: Qu’as-tu à faire de redire mes statuts, et de prendre mon alliance dans ta bouche?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Toi qui hais la correction, et qui as jeté mes paroles derrière toi.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Si tu as vu un voleur, tu t’es plu avec lui, et ta portion est avec les adultères;
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Tu livres ta bouche au mal, et ta langue trame la tromperie;
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Tu t’assieds, tu parles contre ton frère, tu diffames le fils de ta mère:
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Tu as fait ces choses-là, et j’ai gardé le silence; – tu as estimé que j’étais véritablement comme toi; [mais] je t’en reprendrai, et je te les mettrai devant les yeux.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Considérez donc cela, vous qui oubliez Dieu, de peur que je ne déchire, et qu’il n’y ait personne qui délivre.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Celui qui sacrifie la louange me glorifie; et à celui qui règle sa voie je ferai voir le salut de Dieu.

< Zaburi 50 >