< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
A Psalm by Asaph. The Mighty One, God, Yahweh, speaks, and calls the earth from sunrise to sunset.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Out of Zion, the perfection of beauty, God shines out.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Our God comes, and does not keep silent. A fire devours before him. It is very stormy around him.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
He calls to the heavens above, to the earth, that he may judge his people:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
“Gather my saints together to me, those who have made a covenant with me by sacrifice.”
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
The heavens shall declare his righteousness, for God himself is judge. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
“Hear, my people, and I will speak. Israel, I will testify against you. I am God, your God.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
I don’t rebuke you for your sacrifices. Your burnt offerings are continually before me.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
I have no need for a bull from your stall, nor male goats from your pens.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
For every animal of the forest is mine, and the livestock on a thousand hills.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
I know all the birds of the mountains. The wild animals of the field are mine.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
If I were hungry, I would not tell you, for the world is mine, and all that is in it.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Will I eat the meat of bulls, or drink the blood of goats?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Offer to God the sacrifice of thanksgiving. Pay your vows to the Most High.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Call on me in the day of trouble. I will deliver you, and you will honor me.”
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
But to the wicked God says, “What right do you have to declare my statutes, that you have taken my covenant on your lips,
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
since you hate instruction, and throw my words behind you?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
When you saw a thief, you consented with him, and have participated with adulterers.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
“You give your mouth to evil. Your tongue frames deceit.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
You sit and speak against your brother. You slander your own mother’s son.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
You have done these things, and I kept silent. You thought that I was just like you. I will rebuke you, and accuse you in front of your eyes.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
“Now consider this, you who forget God, lest I tear you into pieces, and there be no one to deliver.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Whoever offers the sacrifice of thanksgiving glorifies me, and prepares his way so that I will show God’s salvation to him.”

< Zaburi 50 >