< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
The mighty God, even the LORD, has spoken, and called the earth from the rising of the sun to the going down thereof.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Out of Zion, the perfection of beauty, God has shined.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Our God shall come, and shall not keep silence: a fire shall devour before him, and it shall be very tempestuous round about him.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
He shall call to the heavens from above, and to the earth, that he may judge his people.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Gather my saints together to me; those that have made a covenant with me by sacrifice.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
And the heavens shall declare his righteousness: for God is judge himself. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Hear, O my people, and I will speak; O Israel, and I will testify against you: I am God, even your God.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
I will not reprove you for your sacrifices or your burnt offerings, to have been continually before me.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
I will take no bullock out of your house, nor he goats out of your folds.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
For every beast of the forest is mine, and the cattle on a thousand hills.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
I know all the fowls of the mountains: and the wild beasts of the field are mine.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
If I were hungry, I would not tell you: for the world is mine, and the fullness thereof.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Will I eat the flesh of bulls, or drink the blood of goats?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Offer to God thanksgiving; and pay your vows to the most High:
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
And call on me in the day of trouble: I will deliver you, and you shall glorify me.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
But to the wicked God says, What have you to do to declare my statutes, or that you should take my covenant in your mouth?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Seeing you hate instruction, and casts my words behind you.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
When you saw a thief, then you consented with him, and have been partaker with adulterers.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
You give your mouth to evil, and your tongue frames deceit.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
You sit and speak against your brother; you slander your own mother’s son.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
These things have you done, and I kept silence; you thought that I was altogether such an one as yourself: but I will reprove you, and set them in order before your eyes.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Now consider this, you that forget God, lest I tear you in pieces, and there be none to deliver.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Whoever offers praise glorifies me: and to him that orders his conversation aright will I show the salvation of God.

< Zaburi 50 >