< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
A Psalm of Asaph. God, God, the LORD, hath spoken, and called the earth from the rising of the sun unto the going down thereof.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Out of Zion, the perfection of beauty, God hath shined forth.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Our God cometh, and doth not keep silence; a fire devoureth before Him, and round about Him it stormeth mightily.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
He calleth to the heavens above, and to the earth, that He may judge His people:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
'Gather My saints together unto Me; those that have made a covenant with Me by sacrifice.'
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
And the heavens declare His righteousness; for God, He is judge. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
'Hear, O My people, and I will speak; O Israel, and I will testify against thee: God, thy God, am I.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
I will not reprove thee for thy sacrifices; and thy burnt-offerings are continually before Me.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
I will take no bullock out of thy house, nor he-goats out of thy folds.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
For every beast of the forest is Mine, and the cattle upon a thousand hills.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
I know all the fowls of the mountains; and the wild beasts of the field are Mine.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
If I were hungry, I would not tell thee; for the world is Mine, and the fulness thereof.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Do I eat the flesh of bulls, or drink the blood of goats?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Offer unto God the sacrifice of thanksgiving; and pay thy vows unto the Most High;
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
And call upon Me in the day of trouble; I will deliver thee, and thou shalt honour Me.'
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
But unto the wicked God saith: 'What hast thou to do to declare My statutes, and that thou hast taken My covenant in thy mouth?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Seeing thou hatest instruction, and castest My words behind thee.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
When thou sawest a thief, thou hadst company with him, and with adulterers was thy portion.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Thou hast let loose thy mouth for evil, and thy tongue frameth deceit.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Thou sittest and speakest against thy brother; thou slanderest thine own mother's son.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
These things hast thou done, and should I have kept silence? Thou hadst thought that I was altogether such a one as thyself; but I will reprove thee, and set the cause before thine eyes.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Now consider this, ye that forget God, lest I tear in pieces, and there be none to deliver.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Whoso offereth the sacrifice of thanksgiving honoureth Me; and to him that ordereth his way aright will I show the salvation of God.'

< Zaburi 50 >