< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
A Psalme of Asaph. The God of Gods, euen the Lord hath spoken and called the earth from the rising vp of the sunne vnto the going downe thereof.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Out of Zion, which is the perfection of beautie, hath God shined.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Our God shall come and shall not keepe silence: a fire shall deuoure before him, and a mightie tempest shall be mooued round about him.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Hee shall call the heauen aboue, and the earth to iudge his people.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Gather my Saints together vnto me, those that make a couenant with me with sacrifice.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
And the heauens shall declare his righteousnes: for God is iudge himselfe. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Heare, O my people, and I wil speake: heare, O Israel, and I wil testifie vnto thee: for I am God, euen thy God.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
I wil not reproue thee for thy sacrifices, or thy burnt offerings, that haue not bene continually before me.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
I will take no bullocke out of thine house, nor goates out of thy foldes.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
For all the beastes of the forest are mine, and the beastes on a thousand mountaines.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
I knowe all the foules on the mountaines: and the wilde beastes of the fielde are mine.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
If I bee hungry, I will not tell thee: for the world is mine, and all that therein is.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Will I eate the flesh of bulles? or drinke the blood of goates?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Offer vnto God praise, and pay thy vowes vnto the most High,
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
And call vpon me in the day of trouble: so will I deliuer thee, and thou shalt glorifie me.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
But vnto the wicked said God, What hast thou to doe to declare mine ordinances, that thou shouldest take my couenant in thy mouth,
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Seeing thou hatest to bee reformed, and hast cast my wordes behinde thee?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
For when thou seest a thiefe, thou runnest with him, and thou art partaker with the adulterers.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Thou giuest thy mouth to euill, and with thy tongue thou forgest deceit.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Thou sittest, and speakest against thy brother, and slanderest thy mothers sonne.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
These things hast thou done, and I held my tongue: therefore thou thoughtest that I was like thee: but I will reproue thee, and set them in order before thee.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Oh cosider this, ye that forget God, least I teare you in pieces, and there be none that can deliuer you.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
He that offereth praise, shall glorifie mee: and to him, that disposeth his way aright, will I shew the saluation of God.

< Zaburi 50 >