< Zaburi 50 >
1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
En Psalme af Asaf. Den Almægtige, Gud Herren har talt og kaldet ad Jorden, fra Solens Opgang indtil dens Nedgang.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Fra Zion, Skønhedens Krone, aabenbarede Gud sig herligt.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Vor Gud skal komme og ikke tie; en Ild for hans Ansigt skal fortære, og omkring ham stormer det saare.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Han kalder ad Himmelen oventil og ad Jorden for at dømme sit Folk.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
„Samler mig mine hellige, som have sluttet Pagt med mig ved Offer”.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Og Himlene kundgjorde hans Retfærdighed; thi Gud, han er Dommer. (Sela)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Hør, mit Folk, og jeg vil tale; Israel! og jeg vil vidne imod dig; jeg er Gud, din Gud.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Jeg vil ikke gaa i Rette med dig for dine Slagtofre og for dine Brændofre, som ere altid for mig.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Jeg vil ikke tage en Okse af dit Hus, ej heller Bukke af dine Stalde.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Thi alle Dyrene i Skoven høre mig til, Dyrene paa Bjergene i Tusindtal.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Jeg kender alle Fuglene paa Bjergene, og hvad der vrimler paa Marken, er hos mig.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Dersom jeg hungrede, vilde jeg ikke sige dig det; thi Jorderige hører mig til og dets Fylde.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Skulde jeg vel æde Oksers Kød eller drikke Bukkes Blod?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Offer Gud Taksigelse og betal den Højeste dine Løfter!
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Og kald paa mig paa Nødens Dag; jeg vil udfri dig, og du skal ære mig.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Men til den ugudelige siger Gud: Hvad kommer det dig ved at tale om mine Skikke og at tage min Pagt i din Mund,
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
da du dog hader Tugt og kaster mine Ord bag dig?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Dersom du ser en Tyv, da er du Ven med ham, og med Horkarle er din Del.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Du skikker din Mund til ondt, og med din Tunge digter du Svig.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Du sidder og taler imod din Broder, du sætter Klik paa din Moders Søn.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Disse Ting har du gjort, og jeg har tiet; du har tænkt, at jeg vel var som du; men jeg vil straffe dig og stille det frem for dine Øjne.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Forstaar dog dette, I, som have glemt Gud! at jeg ikke skal rive bort, og der ingen er, som frier.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Den, som ofrer Taksigelse, han ærer mig, og den, som agter paa Vejen, ham vil jeg lade se Guds Frelse.