< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
上主,全能者天主,出令傳召下土,由太陽的出處直到太陽的落處。
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
天主由美麗絕倫的熙雍,發出光明,
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
我們的天主來臨,絕不會默默無聲;吞噬的烈火在祂前面開道,旋轉的風暴在祂的四周怒號。
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
天主呼喚了上乾下坤,要審判自己的人民:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
你們應當給我聚集起虔敬我的人,就是那以犧牲與我訂立盟約的人。
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
諸天要宣示天主的公正,因為祂要親自審判世人。
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
請聽,我的子民,我要發出言語;以色列,我向你警戒告訴,我是天主,我是你的天主。
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
我並不因你的祭獻而責備你,因為我面前常有你的全燔祭。
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
我無須從你的家裏將牛犢攫取,也無須由你的圈裏把羊捉捕;
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
因為,森林裏的種種生物,全歸於我,山陵上的千萬走獸,都屬於我;
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
天空中的一切飛鳥,我都認識,田野間的所有動物,我全知悉。
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
如果我饑餓,我不必向你告訴,因宇宙和其中一切盡屬我有。
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
難道我吃牛犢的肉塊,或者我喝山羊的鮮血?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
為此你該向天主奉獻頌謝祭,你又該向至高者還你的願誓。
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
並在困厄的時日,呼號我,我必拯救你,你要光榮我。
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
天主卻對惡人說:你怎麼膽敢傳述我的誡命,你的口怎敢朗頌我的法令?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
你豈不是惱恨規矩,將我的話置諸腦後?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
你遇見了盜賊,便與他同僚,與犯姦淫的人,就同流合夥;
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
你的口出言不善,你的舌造謠欺騙;
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
不停地毀謗你的兄弟,常污辱你母親的兒子。
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
你既作了這些,我豈能緘口不言?難道你竟以為我真能與你一般¡H我要責斥你,將一切放在你眼前。
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
忘記天主的人們!你們要徹底覺悟,免得我撕裂你們時,沒有人來搶救。
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
奉獻頌謝祭的人就是給我奉獻光榮讚頌,行為正直的人我要使他享見天主的救恩。

< Zaburi 50 >