< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
SI Yuus, junggan, si Yuus, si Jeova sumangan, ya jaagang y tano desde y quinajulo y atdao asta y tumunogña papa güije.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Y sumanjiyong Sion, gosbonito, sí Yuus umiina.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Y Yuusta ufato, ya ti ufamatquilo: y guafe ufanlinachae gui menaña, ya uguaja dangculon pinagyo gui oriyaña.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
uagang gui taquilo na langet yan y tano, para ujusga y taotaoña.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
Nafandaña y mañantos guiya guajo; ayo sija y fumatinas y tratujo pot y inefrese.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Y langet udineclara y tininasña: sa si Yuus güiyaja y jues. (Sila)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
Jingog, O taotaojo, ya jusangan; O Israel, ya bae jusangan testimonio contra jago: guajo si Yuus, ni si Yuusmo.
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
Ti julalatde jao pot y inefresimo, ya y inefresimo sinenggue, para todo y jaane gui menajo.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
Sa ti jufangone nubiyo gui guimamo, ni laje na chiba gui quelatmo.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
Sa todo y gâgâ gui jalom tano, gâjo, yan y gâgâ sija gui jilo y mit na sabana.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Sa jutungo todo y pajaro gui jalom tano; y manmachaleg na gâgâ sija gui jalomtano; todo gâjo.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Yanguin ñalangyo, ti jusanganejao; sa iyoco y tano, yan y sinajguanña.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
Juchoco catnen nubiyo, pat jugui. men jâgâ chiba?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Nae si Yuus inefresen grasia; ya unapase y promesamo gui Gueftaquilo.
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
Ya unagangyo gui jaanen y chinatsaga: junalibrejao, ya siempre unonrayo.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Lao ilegña si Yuus ni y manaelaye; Jafa unfatinas para undeclara y tina. gojo, pat jagas unchule y tratujo gui pachotmo?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Sa jago unchatlie y finanagüe, ya unyute y sinanganjo gui tatemo.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Anae unlie y saque, undalalag güe; yan jagas gaepattejao yan y manábale.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Sa unnasetbe y pachotmo gui tae laye, ya y jilamo fumatitinas ocodon dinague.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Matátachongjao, ya cumuecuentosjao contra y chelumo; undesonra y lajin nanamo.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Estesija finatinasmo, lao mamatquiquilojayo: jinasomo na parejojitja: lao bae julalatdejao, ya jupolo tinaelayemo sija gui menan matamo.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Pago jaso este, jamyo ni y manmalefa as Yuus; na noseaja jusisi jamyo ya jufapidasos, ya taya unalibre.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Y numaeyo inefresen tinina, jaonrayo; ya ayo y munatutunas y sinanganña, jufanue ni y satbasion Yuus.

< Zaburi 50 >