< Zaburi 5 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa filimbi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, tegea sikio maneno yangu, uangalie kupiga kite kwangu.
Escucha, o! Jehová, mis palabras: entiende mi meditación.
2 Sikiliza kilio changu ili unisaidie, Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako ninaomba.
Está atento a la voz de mi clamor, Rey mío, y Dios mío, porque a ti oraré.
3 Asubuhi, unasikia sauti yangu, Ee Bwana; asubuhi naleta haja zangu mbele zako, na kusubiri kwa matumaini.
Jehová, de mañana oirás mi voz: de mañana me presentaré a ti, y esperaré.
4 Wewe si Mungu unayefurahia uovu, kwako mtu mwovu hataishi.
Porque tú no eres Dios que quieres la maldad; el malo no habitará junto a ti.
5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, unawachukia wote watendao mabaya.
No estarán los insensatos delante de tus ojos: a todos los que obran iniquidad, aborreciste.
6 Unawaangamiza wasemao uongo. Bwana huwachukia wamwagao damu na wadanganyifu.
Destruirás a los que hablan mentira: al varón de sangres y de engaño abominará Jehová.
7 Lakini mimi, kwa rehema zako kuu, nitakuja katika nyumba yako, kwa unyenyekevu, nitasujudu kuelekea Hekalu lako takatifu.
Y yo en la multitud de tu misericordia entraré en tu casa: adoraré al santo templo tuyo con tu temor.
8 Niongoze katika haki yako, Ee Bwana, kwa sababu ya adui zangu, nyoosha njia yako mbele yangu.
Jehová, guíame en tu justicia a causa de mis enemigos: endereza delante de mí tu camino.
9 Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika, mioyo yao imejaa maangamizi. Koo lao ni kaburi lililo wazi, kwa ndimi zao, wao hunena udanganyifu.
Porque no hay en su boca rectitud: sus entrañas son pravedades: sepulcro abierto su garganta, con su lengua lisonjearán.
10 Uwatangaze kuwa wenye hatia, Ee Mungu! Hila zao ziwe anguko lao wenyewe. Wafukuzie mbali kwa sababu ya dhambi zao nyingi, kwa kuwa wamekuasi wewe.
Asuélales, o! Dios, caigan de sus consejos: por la multitud de sus rebeliones échales, porque se rebelaron contra ti.
11 Lakini wote wakimbiliao kwako na wafurahi, waimbe kwa shangwe daima. Ueneze ulinzi wako juu yao, ili wale wapendao jina lako wapate kukushangilia.
Y alegrarse han todos los que esperan en ti; para siempre se regocijarán, y cubrirles has, y alegrarse han en ti los que aman tu nombre.
12 Kwa hakika, Ee Bwana, unawabariki wenye haki, unawazunguka kwa wema wako kama ngao.
Porque tú bendecirás al justo, o! Jehová; como de un pavés le cercarás de benevolencia.