< Zaburi 5 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa filimbi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, tegea sikio maneno yangu, uangalie kupiga kite kwangu.
Al maestro del coro. Per flauti. Salmo. Di Davide. Porgi l'orecchio, Signore, alle mie parole: intendi il mio lamento.
2 Sikiliza kilio changu ili unisaidie, Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako ninaomba.
Ascolta la voce del mio grido, o mio re e mio Dio, perché ti prego, Signore.
3 Asubuhi, unasikia sauti yangu, Ee Bwana; asubuhi naleta haja zangu mbele zako, na kusubiri kwa matumaini.
Al mattino ascolta la mia voce; fin dal mattino t'invoco e sto in attesa.
4 Wewe si Mungu unayefurahia uovu, kwako mtu mwovu hataishi.
Tu non sei un Dio che si compiace del male; presso di te il malvagio non trova dimora;
5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, unawachukia wote watendao mabaya.
gli stolti non sostengono il tuo sguardo. Tu detesti chi fa il male,
6 Unawaangamiza wasemao uongo. Bwana huwachukia wamwagao damu na wadanganyifu.
fai perire i bugiardi. Il Signore detesta sanguinari e ingannatori.
7 Lakini mimi, kwa rehema zako kuu, nitakuja katika nyumba yako, kwa unyenyekevu, nitasujudu kuelekea Hekalu lako takatifu.
Ma io per la tua grande misericordia entrerò nella tua casa; mi prostrerò con timore nel tuo santo tempio.
8 Niongoze katika haki yako, Ee Bwana, kwa sababu ya adui zangu, nyoosha njia yako mbele yangu.
Signore, guidami con giustizia di fronte ai miei nemici; spianami davanti il tuo cammino.
9 Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika, mioyo yao imejaa maangamizi. Koo lao ni kaburi lililo wazi, kwa ndimi zao, wao hunena udanganyifu.
Non c'è sincerità sulla loro bocca, è pieno di perfidia il loro cuore; la loro gola è un sepolcro aperto, la loro lingua è tutta adulazione.
10 Uwatangaze kuwa wenye hatia, Ee Mungu! Hila zao ziwe anguko lao wenyewe. Wafukuzie mbali kwa sababu ya dhambi zao nyingi, kwa kuwa wamekuasi wewe.
Condannali, o Dio, soccombano alle loro trame, per tanti loro delitti disperdili, perché a te si sono ribellati.
11 Lakini wote wakimbiliao kwako na wafurahi, waimbe kwa shangwe daima. Ueneze ulinzi wako juu yao, ili wale wapendao jina lako wapate kukushangilia.
Gioiscano quanti in te si rifugiano, esultino senza fine. Tu li proteggi e in te si allieteranno quanti amano il tuo nome.
12 Kwa hakika, Ee Bwana, unawabariki wenye haki, unawazunguka kwa wema wako kama ngao.
Signore, tu benedici il giusto: come scudo lo copre la tua benevolenza.

< Zaburi 5 >