< Zaburi 5 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa filimbi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, tegea sikio maneno yangu, uangalie kupiga kite kwangu.
大衛的詩,交與伶長。用吹的樂器。 耶和華啊,求你留心聽我的言語, 顧念我的心思!
2 Sikiliza kilio changu ili unisaidie, Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako ninaomba.
我的王我的上帝啊,求你垂聽我呼求的聲音! 因為我向你祈禱。
3 Asubuhi, unasikia sauti yangu, Ee Bwana; asubuhi naleta haja zangu mbele zako, na kusubiri kwa matumaini.
耶和華啊,早晨你必聽我的聲音; 早晨我必向你陳明我的心意,並要警醒!
4 Wewe si Mungu unayefurahia uovu, kwako mtu mwovu hataishi.
因為你不是喜悅惡事的上帝, 惡人不能與你同居。
5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, unawachukia wote watendao mabaya.
狂傲人不能站在你眼前; 凡作孽的,都是你所恨惡的。
6 Unawaangamiza wasemao uongo. Bwana huwachukia wamwagao damu na wadanganyifu.
說謊言的,你必滅絕; 好流人血弄詭詐的,都為耶和華所憎惡。
7 Lakini mimi, kwa rehema zako kuu, nitakuja katika nyumba yako, kwa unyenyekevu, nitasujudu kuelekea Hekalu lako takatifu.
至於我,我必憑你豐盛的慈愛進入你的居所; 我必存敬畏你的心向你的聖殿下拜。
8 Niongoze katika haki yako, Ee Bwana, kwa sababu ya adui zangu, nyoosha njia yako mbele yangu.
耶和華啊,求你因我的仇敵,憑你的公義引領我, 使你的道路在我面前正直。
9 Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika, mioyo yao imejaa maangamizi. Koo lao ni kaburi lililo wazi, kwa ndimi zao, wao hunena udanganyifu.
因為,他們的口中沒有誠實; 他們的心裏滿有邪惡; 他們的喉嚨是敞開的墳墓; 他們用舌頭諂媚人。
10 Uwatangaze kuwa wenye hatia, Ee Mungu! Hila zao ziwe anguko lao wenyewe. Wafukuzie mbali kwa sababu ya dhambi zao nyingi, kwa kuwa wamekuasi wewe.
上帝啊,求你定他們的罪! 願他們因自己的計謀跌倒; 願你在他們許多的過犯中把他們逐出, 因為他們背叛了你。
11 Lakini wote wakimbiliao kwako na wafurahi, waimbe kwa shangwe daima. Ueneze ulinzi wako juu yao, ili wale wapendao jina lako wapate kukushangilia.
凡投靠你的,願他們喜樂,時常歡呼, 因為你護庇他們; 又願那愛你名的人都靠你歡欣。
12 Kwa hakika, Ee Bwana, unawabariki wenye haki, unawazunguka kwa wema wako kama ngao.
因為你必賜福與義人; 耶和華啊,你必用恩惠如同盾牌四面護衛他。