< Zaburi 48 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Grande es el Señor y grandemente digno de ser alabado, en la ciudad de nuestro Dios, en su santo monte.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Hermosa provincia, la alegría de toda la tierra, es la montaña de Sión, haya en el extremo norte, la montaña de Dios, la ciudad del gran Rey.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
En sus palacios, Dios es conocido como una torre fuerte.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Para ver los reyes se unieron por acuerdo, se unieron y avanzaron contra ella.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Ellos vieron la ciudad. y estaban llenos de asombro; se turbaron y huyeron con miedo.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
El miedo se adueñó de ellos los sacudió y sufrieron dolor, como en una mujer en el parto.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Por ti las naves de Tarsis están quebradas como por un viento del este.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Cómo llegó a nuestros oídos, así lo hemos visto, en la ciudad del Señor de los ejércitos, en la ciudad de nuestro Dios; Dios la afirmará para siempre. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Nos acordamos de tu misericordia, oh Dios, mientras estábamos en tu Templo.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Como corresponde a tu nombre, oh Dios, así es tu alabanza hasta lo último de la tierra; tu diestra está llena de justicia.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Que haya alegría en el monte de Sion, y que se alegren las hijas de Judá, por tus sabias decisiones.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Sigue tu camino por Sión, dale la vuelta y enumera sus torres.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Tome nota de sus fuertes muros, mirando bien sus palacios; para que le cuentes a la generación que viene después.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Porque este Dios es nuestro Dios por los siglos de los siglos: él será nuestro guía eternamente.