< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Canción: Salmo de los hijos de Coré. GRANDE es Jehová y digno de ser en gran manera alabado, en la ciudad de nuestro Dios, en el monte de su santuario.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Hermosa provincia, el gozo de toda la tierra es el monte de Sión, á los lados del aquilón, la ciudad del gran Rey.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
Dios en sus palacios es conocido por refugio.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Porque he aquí los reyes de la tierra se reunieron; pasaron todos.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
Y viéndola ellos así, maravilláronse, se turbaron, diéronse priesa [á huir].
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Tomólos allí temblor; dolor, como á mujer que pare.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
Con viento solano quiebras tú las naves de Tharsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Como [lo] oímos, así hemos visto en la ciudad de Jehová de los ejércitos, en la ciudad de nuestro Dios: afirmarála Dios para siempre. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Esperamos tu misericordia, oh Dios, en medio de tu templo.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Conforme á tu nombre, oh Dios, así es tu loor hasta los fines de la tierra: de justicia está llena tu diestra.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Alegraráse el monte de Sión; se gozarán las hijas de Judá por tus juicios.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Andad alrededor de Sión, y rodeadla: contad sus torres.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Poned vuestro corazón á su antemuro, mirad sus palacios; para que lo contéis á la generación venidera.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
Porque este Dios es Dios nuestro eternalmente y para siempre: él nos capitaneará hasta la muerte.

< Zaburi 48 >