< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
Cántico. Salmo de los hijos de Coré. Grande es Yahvé en la ciudad de nuestro Dios, y digno de suma alabanza.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Su monte sagrado es gloriosa cumbre, es el gozo de toda la tierra; el monte Sión, (su) extremo norte, es la ciudad del gran Rey.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
En sus fortalezas, Dios se ha mostrado baluarte seguro.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
Pues, he aquí que los reyes se habían reunido, y acometieron a una;
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
mas apenas le vieron, se han pasmado, y aterrados han huido por doquier.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Los invadió allí un temblor, una angustia como de parto,
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
como el viento de Oriente cuando estrella las naves de Tarsis.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
Como lo habíamos oído, así lo hemos visto ahora en la ciudad de Yahvé de los ejércitos, en la ciudad de nuestro Dios: Dios la hace estable para siempre.
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
Nos acordamos, oh Dios, de tu misericordia dentro de tu Templo.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
Como tu Nombre, Dios, así también tu alabanza llega hasta los confines de la tierra. Tu diestra está llena de justicia.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Alégrese el monte Sión; salten de júbilo las ciudades de Judá, a causa de tus juicios.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Recorred a Sión, circulad en rededor, contad sus torres;
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
considerad sus baluartes, examinad sus fortalezas, para que podáis referir a la generación venidera: así es de grande Dios,
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
nuestro Dios para siempre jamás. Él mismo nos gobernará.

< Zaburi 48 >